Skip to main content
๐Š๐”๐™๐Ž๐‘๐Ž๐“๐€ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐ˆ๐”๐๐ƒ๐Ž๐Œ๐๐ˆ๐๐” ๐๐€ ๐‡๐”๐ƒ๐”๐Œ๐€ ๐Š๐€๐“๐ˆ๐Š๐€ ๐‰๐„๐๐†๐Ž ๐‹๐€ ๐๐ˆ๐Œ๐€ ๐“๐Ž๐–๐„๐‘๐’ โ€“ ๐Š๐€๐”๐๐“๐ˆ ๐˜๐€ ๐Œ๐Ž๐Œ๐๐€๐’๐€

๐Š๐”๐™๐Ž๐‘๐Ž๐“๐€ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐ˆ๐”๐๐ƒ๐Ž๐Œ๐๐ˆ๐๐” ๐๐€ ๐‡๐”๐ƒ๐”๐Œ๐€ ๐Š๐€๐“๐ˆ๐Š๐€ ๐‰๐„๐๐†๐Ž ๐‹๐€ ๐๐ˆ๐Œ๐€ ๐“๐Ž๐–๐„๐‘๐’

Seneta wa Kaunti ya Mombasa, Mohamed Faki ameomba Kauli kutoka kwa Kamati ya Kudumu ya Barabara, Uchukuzi na Makao kuhusu kuzorota kwa miundombinu na huduma katika Jengo la โ€˜Bima Towersโ€™ katika Kaunti ya Mombasa.

Seneta Faki ameiomba Kamati hiyo ichunguze na kuripoti katika Seneti sababu zilizopelekea lifti katika jengo hilo kutofanya kazi kwa muda wa zaidi ya miaka miwili pamoja pia na ukosefu wa huduma ya maji safi katika jengo hilo, ikizingatiwa kwamba jumba hilo lina ofisi mbalimbali za Serikali ya Kaunti ya Mombasa, ambapo mamia ya watu huzuru kila siku kutafuta huduma za dharura.

Kamati hio pia inahitajika iarifu Seneti chanzo cha utepetevu katika usimamizi wa jengo hilo, ikizingatiwa kwamba jengo hilo lilikabidhiwa Serikali kipindi kifupi tu kilichopita.